Monday, September 24, 2012

EMMYS AWARDS 2012: RED CARPET




CHELSEE HEALEY ROCKS LEATHER PEPLUM TROUSERS



HAPPY ONE YEAR WEDDING ANNIVERSARY MY SWEET LOVE

 Sasa umetimia Mwaka tokea tuanze maisha ya kuishi pamoja
WITH MY HUSBAND
 NAMPENDA SANA MUME WANGU
 MR. & MRS. CATHBERT ANGELO 
 Naamini Milima na mabonde tutayavuka hadi Mwenyezi Mungu atakaposema ya kwake
 Alituachia Amri Kuu ya Mapendo, inatupasa kuendelea....palipo na upendo kusikilizana kupo, kufundishana kupo, kurekebishana kupo, kuburudishana kupo, nk.
 Siku zote 2 si sawa na 1, sijutii kuwa ndani ya Ndoa
Mungu ni mwema siku zote.......Namtja sana Mungu kwani ndiye ametuweka hadi leo na Mema yote twayategemea kutoka kwake.

MAY GOD BLESS US ABUNDANTLY... ........AMEN

Saturday, September 22, 2012

SEND OFF PARTY YA VERONICA NDANI YA MANJU MSITA DESIGNS ....20/09/2012 UKUMBI WA STUDENT CENTRE TABORA

 Watoto wawili Walifungua njia kwa kumwaga maua na show ya kupendeza
 Madada na Makaka tukafuata kwa Show Maalumu
Bibi Harusi mratajiwa Veronica Stima akiwa amesindikiza na kaka yake John Stima kuingia katika ukumbi kwa ajili ya sherehe ya kumuaga (Send Off) iliyofanyika Student Centre, Tabora. Ambapo Harusi yake ni Jumamosi Septemba 22, 2012.
Tulifuata kwa show ya pamoja na Bibi harusi mtarajiwa
 Baba na mama yake mzazi Veronica Stima (kutoka kulia) wakicheza wimbo wa kabila la Kifipa.
 Wakwe wa bibi harusi mtarajiwa wakiingia ukumbini kwa madaha.
 Bi Harusi mtarajiwa Veronica Stima akiwa na kaka na dada zake waliomsindikiza katika sherehe yake ya send off iliyofanyika ukumbi wa Student Centre, Tabora.
 Bibi Harusi Mtarajiwa Veronica Stima akimlisha mtarajiwa wake Bw. Allen Mnene
Wachaga nao hawakuwa nyuma kuonyesha umoja wao na ule wimbo wao wa kushikana mikono.
 Bwana harusi mtarajiwa Allen na mkewe mtarajiwa Veronica Stima wakienda mbele kwa ajili ya utambulisho.
 ...akilishwa keki na mtarajiwa wake
 Bibi harusi mtarajiwa akiaga wazazi wake, kujitayarisha kuungana na mwenzake
 ...hapa bibi harusi mtarajiwa alikuwa akitoa keki kwa mama mkwe wake mtarajiwa huku kaka yake akiwa amemsindikiza.
 
Mzee Prosper Stima ambaye ni baba wa bibi harusi mtarajiwa akitoa machache.
Mama Catherine Stima ambaye ni mama mazazi wa bibi harusi nae alipata wasaa wa kutoa machache kwa mwanae.
 Kaka mkubwa John Stima akiongea machache kabla ya kumkabidhi dada yake kwa shemeji zake. Alisema, 'Nawakabidhi dada yangu mpendwa, hana hata doa... nawaombeni msije mkanyanyasa'.
 
...mara baada ya kuongea machache kaka mkubwa alikabidhiwa begi la nguo za bibi harusi, tayari kwa maandalizi ya harusi.
 Aha... Bwana na Bibi Cathbert Angelo nao walikuwepo kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa.
Bibi harusi mratajiwa (wapili kutoka kulia) akiwa na dada zake.
 Muda wa kupata show ulifika na mambo yalikuwa kama unavyoona mwenyewe....tulibadili tukavaa viatu maalumu vya show
Picha ya kumbu kumbu kwa wake na watoto wao. Nguo zote za shughuli hiyo zimedizainiwa na na kushonwa na mwanamitindo Manju Msita
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...